Friday, July 5, 2013

TUTAWEZAJE KUPUNGUZA WIMBI LA WATU WANAOJAZANA DAR BILA SHUGHULI MAALUM BILA KUANGALIA CHIMBUKO LA WANAPOTOKEA?

Kiukweli maisha halisi ya watanzania wengi tunapotokea maisha yetu ni ya hali ya chini sana ila unafichwa na ule msemo unaosema umaridadi huficha umasikini. Japo nilizaliwa na kukulia Dar kwenye familia ya maisha ya kawaida sana lakini mara tu baada ya kutoka kwenda Iringa niliposoma kidato cha tano na sita katika shule ya Sekondari Malangali hapo ndipo nilipobahatika kuona maisha halisi ya huyu Mtanzania baada ya kuzunguka vijiji mbalimbali katika Mkoa huo wa Iringa.


Nashukuru Mungu nilimaliza masomo yangu na sasa nipo mkoani Tabora kikazi. Kwa miaka 2 tu niliyoishi huku inatosha kujua kwa nini watu wanakimbilia Dar kiukweli maisha ya watu wengi huku ni ya hali ya chini japo mji ni mkongwe na una historia kubwa. Mzunguko wa pesa ni mgumu sana kitu kidogo tu uatazunguka kukipata na ukikipata hiyo bei yake sasa ukiuliza nini utaambiwa gharama za usafirishaji ziko juu. Tumeshazoea kuona mijini majengo ya maana lakini huku unapoingia tu unakutana na nyumba kongwe za tope. Mbaya zaidi mbunge husika yuko Dar yeye kila siku migogoro kwenye klabu kongwe ya mpira wa miguu ya Simba hata siku moja sijawahi kumsikia akielezea matatatizo wa wananchi wake waliompigia kura.

Sikuishia hapo kutokana na kazi yangu nimeweza kutembelea baadhi ya vijiji wilaya mbalimbali za mkoa huu. Huko ndio hakutamaniki maisha yao ni magumu na ya hali ya chini sana lakini kubwa lililonigusa hadi kuandika makala hii ni hishoria ya mtoto mmoja aitwaye Asha Alfred. Mama yake na baba yake wametengana mama yuko mjini na baba ni mfugaji yuko kijijini hivyo mtoto kachukuliwa na baba ambaye ana familia mbili ambazo ziko vijiji tofauti. Mtoto huyu amepelekwa kwa mke mdogo kijiji kingine tofauti na anachoishi huyu baba. kijiji chenyewe kipo mbali na huduma za jamii ni mwendo wa kutosha kutoka nyumba moja hadi kumkuta jirani.
Asha akiwa na familia yake na mama yake mzazi alipomtembelea

Asha akiwa na familia yake nyuma aliyesimama ni mke mdogo wa baba yake ndiye ambae anaishi na asha kwa sasa

Maisha ya mtoto huyu ambaye alikuwa tayari ameanza shule ya awali alipokuwa mjini sasa yamekuwa ni ya ufugaji ambayo hayana tena future ya kupata haki yake ya msingi ambayo ni elimu.Na hata kama akiandikishwa bado itakuwa mateso kwake kwani ni umbali mrefu wa kukakiza mapori mpaka kuikuta shule ya msingi ilipo. Lakini haya ndio maisha yetu ya kila siku na wengi wetu tulipotokea japo huwa hatupendi kuzungumzia mara tu tunapopata mafanikio. 

Je unafikiri mtu kama huyu anapopata nafasi ya kufika Dar hata kama hatokuwa na pa kulala unadhani atatamani kurudi tena huku kijijini ambako haoni hata future yake?


Picha za Asha akiwa anachunga ng'ombe

Mdogo wake Asha (Story & photo by Timothy Mwakimbwala)





Wednesday, October 5, 2011

KUTANA NA MCHUNGAJI MUSA ASKARI ALIYEAJILIWA JESHI LA SERIKALI YA MBINGUNI KIKOSI CHA MIZINGA ANAVYOILIPUA TABORA

Mchugaji Musa

One 2 one Interview by Timothy Mwakimbwala.


Mwandishi: Bwana asifiwe Mchungaji, za uzima?
Mchungaji: Amina, tunamshukuru Mungu kwa kuwa wazima wa afya maana kuna wengi walitamani kuwepo leo lakini hawakuweza kuamka.

Mwandishi: Mchungaji naweza kujua historia yako kwa ufupi?
Mchungaji: kwa jina naitwa Mchungaji Musa Sheka Makala natambulika zaidi kama askari kutoka jeshi la serikali ya mbinguni kikosi cha mizinga. Nilizaliwa mwaka 1982 mkoa wa Singida wilayani Iramba katika kijii cha Makunda.

Mwandishi: Asante sana kwa historia yako sasa ilikuwajekuwaje mpaka ukajikuta umeajiliwa kama askari wa jeshi la serikali ya mbinguni katika kikosi cha mizinga?
Mchungaji: (Anacheka kidogo) Mnamo mwaka 2005 nilisikia mungu akisema nami nikiwa Igunga mkoani Tabora. Ikatokea katika kanisa nililokuwa nasali alikumja Mchungaji kutoka Dar es salaam Mchungaji Martin kuhudumu kwenye semina baada ya semina kumalizika aliniomba twende wote Dar es salaam. Huko nilianza kwa kuombea wagonjwa mahospitalini hasa hospitali ya Taifa ya Muhimbili na nikaanza kujifunza kuhuburi chini ya mwalimu wangu mchungaji Martini. Mnamo 2006 nikaenda kufungua kanisa moshi mkoani Kilimanjaro. Ki ukweli huko nilimuona Mungu kwani kwa siku ya kwanza tu niliweza kupata washirika 35. Huko nilidumu kwa mwaka mmoja na ilipofika 2007 nikarudi tena Dar es salaam kuendelea na huduma. Nilipofika Dar es salaam safari hii nikaanza kupata mihaliko ya mikutano na semina toka sehemu mbalimbali za Tanzania.

Mwandishi: Katika huduma yako ulishawahi kuifikia mikoa ipi?
Mchungaji: Mpaka sasa nimeshatembelea Dar es salaam, Kilimanjaro, Arusha, Singida, Shinyanga, Mwanza, Dodoma, Mtwara, Lindi, Tanga na Tabora.


Mwandishi: Ilikuwajekuwaje mpaka ukaamua kuweka kambi Tabora?
Mchungaji: Mtumishi wa Mungu Mchungaji Lutengano Mwasongela baada ya kusikia habari zangu aliamua kunitafuta na kuniomba nije kuwa mchungaji mzaidizi katika kanisa lake lililo chini ya TAG, linalojulikana kama TAG Maranatha Miracle Centre lililopopo Cheyo B Tabora mjini. Nakumbuka hiyo ilikuwa 2010 mwezi wa nne ndipo nilipofika hapa na ndipo napohudumu mpaka sasa.


Mwandishi: Ni mtumishi gani unayempenda hapa Tanzania na ungependa kuwapa ushauri gani watumishi wa Mungu?
Mchungaji: Kiukweli mimi nampenda sana Mwalimu Mwakasege jinsi anavyofundisha. Cha kuwashauri watumishi wa Mungu ambao Mungu amewaita wanatakiwa wakae chini ya Mungu na kumsikiliza roho wa Mungu awape cha kusema katika ulimwengu wa sasa na ndipo watakapoinuliwa kwenda viwango vingine.

Mwandishi: Asante sana mchungaji kwa ushirikiano wako uliouonyesha na Mungu akubariki sana.

Mchungaji: Amina, nashukuru sana na karibu tena siku nyingine ukiwa na lolote Mungu akubariki sana.
Mchungaji Musa akiwa ofisini

Huyu ndio Mchungaji Musa ambaye anahubiri kila jumamosi saa 2:30 Usiku katika kipndi cha Usilie tena C.G fm. Ukiwa na shida za Maombezi na Ushauri Mchungaji Musa pamoja na Mchungaji kiongozi Mchungaji Lutengano Mwasongela wanapatikana ofisini katika kanisa la TAG Maranatha Miracle Centre lililopo Cheyo B Tabora Mjini kila siku kuanzia Jumatatu hadi Jumamosi saa 4 hadi saa 12 jioni.

  Kwa mawasiliano piga: 0788-495870
                                         0762-111492  
                                          0652-364772
Mchungaji musa akiwa ofisini
Mchungaji Musa akiwa na Eliud Moses Mhasibu wa Compassion

Thursday, September 29, 2011

MKALI WA COMEDY ALIYETOKA KAOLE ARTS GROUP MPAKA FPA UDSM

Idara ya sanaa chuo kikuu Dar es salaam chimbuko la vipaji


Na Timothy Mwakimbwala
Anajulikana kama Ujio Netho wengi wanamfaamu kama Ujio ndio jina alilozoea kulitumia kwenye tamthilia mbalimabali alizocheza. Ni msanii ambaye ameibuka kwa kasi ya ajabu kwenye tasnia ya uigizaji bongo. Nafasi anazopendelea kucheza ni za uchekeshaji ambazo anaonekana kuzimudu kwa kiwango cha juu. Ujio ni msanii toka kundi kongwe la sanaa nchini linajulikana kama Kaole sanaa group ambalo limewatoa mastaa kibao wanaofanya vema kwenye kiwanda cha filamu bongo kama Ray, kanumba , Johari, Tino, tea na wakali wengine kibao

Ujio netho
Unapomkuta nje ya fani ya uigizaji ni mtu mmoja mpole ambaye bila kuwahi kumuona unapoambiwa habari zake huwezi kuamini. Lakini ukweli ni kwamba huyo ndio Ujio Netho kijana mwenye vituko kupitiliza awapo kazini. Ujio kwa sasa anamalizia mwaka wake wa tatu katika chuo kikuu cha Dar es salaam ambapo alijiunga toka mwaka 2009 ili kukiendeleza kipaji chake cha uchekeshaji.
Ujio Netho akiwa na Bambo mkongwe wa comedy zao kutoka kaole sanaa group
ujio Netho katika pozi

Saturday, September 24, 2011

BIG SHAH A.K.A THE BIG PRODUCER MKALI WA MUZIKI TOKA FPA (UDSM) ALIYEANGUKIA KWENYE BONGO MOVIES

Na Timothy Mwakimbwala
Anajulikana kama Big Shah kutokana na kuwa na mwili mkubwa ni mzaliwa wa Dar es salaam. Ni kijana aliyebalikiwa kuwa na vipaji vingi. Mwaka 2008 akitokea Shule alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es salaam akitafuta shahada ya sanaa (Fine & Peforming Arts), akitaka kukiendeleza kipaji chake cha Utengenezaji Muziki (Producer). Big Shah ameshawahi kuwatoa wasanii chipukizi kibao akiwemo Richard Nyandindi na wengineo wakati huo akiwa producer jijini Mbeya.
.
Big Shah akiwa darasa la Muziki FPA akipiga saxaphone

Big Shah akiwa katika darasa la muziki FPA (UDSM) akijifunza kupiga gitaa. By Timothy Mwakimbwala
Big Shah akiwa studio akitengeneza Muziki

 Big shah kwa sasa amemaliza shahada yake ya kwanza ya sanaa (BA in Fine & Performing Arts) katika chuo kikuu cha Dar es salaam. Pamoja na ugalacha wake wote kwenye tasnia ya muziki aliamua kuweka mikoba pembeni kidogo na kujiingiza kwenye Bongo Movies ambapo kwa sasa ameamua kufungua kampuni yake inayojulikana kama  Natives Filmes.

Big Shah akiwa na camera akishoot  Documentary
Big Shah aliyeshika camera akiwa mzigoni kushoot filamu
Huyu ndio Big Shah mkali wa Muziki  toka kiwanda cha vipaji FPA anayetingisha ndani ya Bongo Movies akiwa mzigoni kwenye kutengeneza filamu. By Timothy Mwakimbwala

Friday, September 23, 2011

RICHARD NYANDINDI MGODI MPYA WA HIP HOP TOKA FPA (UDSM) UNAOTEMA MAWE KWA KASI NDANI YA ULIMWENGU WA HIP HOP BONGO

Na Timothy Mwakimbwala.

Anaitwa Richard Nyandindi mzaliwa wa Dar es salaam. Ni mkali wa michano anayeusudu MIC kuliko kitu chochote. Alianza kujulikana kwa kupanda kwenye maconcert wakati huo akiwa anasoma Mbalizi sec school iliyoko Mbeya.Kwa kuwa sanaa ipo damuni aliamua kujiunga chuo kikuu cha Dar er salaam ili kusomea shahada ya sanaa (Fine & Performing Arts) akifuata nyayo za aliyekuwa Producer wake wakati huo akitokea Mbeya, hapa namamzungumzia Big Shah.

Richard Nyandindi kwa sasa yuko mbioni kuachia kibao chake kipya kinachoitwa ABC akimshirikisha wa jina wake Philipo Nyandindi O-TEN. Wapenzi wa Hip Hiop kaeni mkao wa kula kusikiliza ngoma kali ya Richard Nyandindi
                                               Richard Nyandindi akiwa katika pozi toauti.

The former Producer wa Richard Nyandindi Big Shah a.k.a Shah Native the big producer akiwa mtamboni. Photo by Timothy Mwakimbwala.

Friday, September 16, 2011

EVA CHARLES KALUNDE ALMASI ILIYOJIFICHA MCHANGANI..........!

 Na Timothy A. Mwakimbwala.
Anaitwa Eva Charles Kalunde ni mzaliwa wa Tabora.Ni lulu mpya kwenye tasnia ya muziki was Injili. Mbio zake za usanii zilianza kukomaa alipokuwa sekondari. Wakati huo akiwa anasoma shule ya sekondari Mwinyi iliyopo Tabora mjini. Alianza kujulikana kwa kuimba kwenye makutano ya wanafunzi maarufu kama "joint mass" zinazowakutanisha wanafunzi wa shule mbalimbali za Tabora. Hapo ndipo alipokutana na wanafunzi wenzake Mariam Joseph Kariuk na Martha Tiluli ambapo kwa pamoja waliamua kuanzisha band iliyojulikana kama Doxa Band.

Baada ya kuanzisha band hiyo ndipo walipoamua kumtafuta mlezi ambapo kwa pamoja waliamua kujiunga na kanisa TAG Maranatha Miracle Centre lililopo Cheyo B Tabora mjini chini ya Mchungaji Lutengano Mwasongela ambaye aliamua kuubeba mzigo huo na kuwa mlezi wao.
Eva Charles ni almasi iliyojificha kwa sababu si kitu cha kawaida kwa mtu mwenye kipaji cha kweli kama cha Eva kutovuma angalau tu kwa mkoa wa Tabora. Mara ya kwanza nilipomuona akiimba pamoja na band yao katika kanisa a TAG Maranatha Miracle Centre haikuwa rahisi kuamini kwamba nyimbo walizokua wanaimba ilikuwa ni live band. Kwani waliimba nyimbo zao kwa ustadi mkubwa kana kwamba walikuwa wanatumia back up CD. Na haikuwa rahisi kuamini kwamba hawakuwahi kurekodi hata albamu moja.

Eva Charles kwa sasa amemaliza kidato cha sita katika shule ya sekondari Uyui iliyopo pia Tabora mjini. Ndoto zake kimaisha ni siku moja kuwa msanii wa kimataifa wa muziki wa Injili na kuwa msomi mkubwa. Ili kutimiza hilo kwa sasa anatarajia kujiunga na chuo kikuu kwa mwaka wa masomo 2011/2012 kwa ajili ya kuitafuta shahada yake ya kwanza.
                            Huyu ndio Eva Charles Kalunde zao kutoka TAG Maranatha Miracle Centre lilopo Cheyo B (Tabora mjini) kwa Mchungaji kiongozi Mchungaji Lutengano Mwasongela.

Saturday, September 10, 2011

TAG MARANATHA MIRACLE CENTRE "Cheyo B" Tabora Mjini

Mchungaji kionngozi wa kanisa la TAG Maranatha Miracle Centre lililopo Cheyo B karibu na shule ya msingi Cheyo B (Tabora Mjini), Pastor Lutengano Mwasongela anapenda kuwakaribisha kwenye Ibada ya Miujiza inayofanyika kila jumapili kuanzia saa 3 asubuhi na kuendelea. Na kwa huduma ya maombezi na ushauri Mchungaji kiongozi na jopo lake la wachungaji anapatikana kila siku ofisini kwake kanisani hapo kuanzia saa 3 hadi saa 12 jioni. mnakaribishwa wakazi wote wa Tabora na vitongoji vyake.