Saturday, September 24, 2011

BIG SHAH A.K.A THE BIG PRODUCER MKALI WA MUZIKI TOKA FPA (UDSM) ALIYEANGUKIA KWENYE BONGO MOVIES

Na Timothy Mwakimbwala
Anajulikana kama Big Shah kutokana na kuwa na mwili mkubwa ni mzaliwa wa Dar es salaam. Ni kijana aliyebalikiwa kuwa na vipaji vingi. Mwaka 2008 akitokea Shule alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es salaam akitafuta shahada ya sanaa (Fine & Peforming Arts), akitaka kukiendeleza kipaji chake cha Utengenezaji Muziki (Producer). Big Shah ameshawahi kuwatoa wasanii chipukizi kibao akiwemo Richard Nyandindi na wengineo wakati huo akiwa producer jijini Mbeya.
.
Big Shah akiwa darasa la Muziki FPA akipiga saxaphone

Big Shah akiwa katika darasa la muziki FPA (UDSM) akijifunza kupiga gitaa. By Timothy Mwakimbwala
Big Shah akiwa studio akitengeneza Muziki

 Big shah kwa sasa amemaliza shahada yake ya kwanza ya sanaa (BA in Fine & Performing Arts) katika chuo kikuu cha Dar es salaam. Pamoja na ugalacha wake wote kwenye tasnia ya muziki aliamua kuweka mikoba pembeni kidogo na kujiingiza kwenye Bongo Movies ambapo kwa sasa ameamua kufungua kampuni yake inayojulikana kama  Natives Filmes.

Big Shah akiwa na camera akishoot  Documentary
Big Shah aliyeshika camera akiwa mzigoni kushoot filamu
Huyu ndio Big Shah mkali wa Muziki  toka kiwanda cha vipaji FPA anayetingisha ndani ya Bongo Movies akiwa mzigoni kwenye kutengeneza filamu. By Timothy Mwakimbwala

No comments:

Post a Comment