Na Timothy Mwakimbwala.
Anaitwa Richard Nyandindi mzaliwa wa Dar es salaam. Ni mkali wa michano anayeusudu MIC kuliko kitu chochote. Alianza kujulikana kwa kupanda kwenye maconcert wakati huo akiwa anasoma Mbalizi sec school iliyoko Mbeya.Kwa kuwa sanaa ipo damuni aliamua kujiunga chuo kikuu cha Dar er salaam ili kusomea shahada ya sanaa (Fine & Performing Arts) akifuata nyayo za aliyekuwa Producer wake wakati huo akitokea Mbeya, hapa namamzungumzia Big Shah.
Richard Nyandindi kwa sasa yuko mbioni kuachia kibao chake kipya kinachoitwa ABC akimshirikisha wa jina wake Philipo Nyandindi O-TEN. Wapenzi wa Hip Hiop kaeni mkao wa kula kusikiliza ngoma kali ya Richard Nyandindi
Richard Nyandindi akiwa katika pozi toauti.
The former Producer wa Richard Nyandindi Big Shah a.k.a Shah Native the big producer akiwa mtamboni. Photo by Timothy Mwakimbwala.
No comments:
Post a Comment